JINSI ya Kujisajili na Kutuma Maombi ya Kazi Kupitia Ajira Portal
JINSI ya Kujisajili na Kutuma Maombi ya Kazi Kupitia Ajira Portal
Mfumo wa Ajira wa Serikali ni Mfumo unaopokea Maombi Mbalimblai kila Siku kwa nafasi zinazotangazwa na sekretarieti ya ajira UTUMISHI na Utawala Bora.
Katika Makala hii utajifunza Jinsi ya Kujisajili Katika Tovuti ya Ajira Tanzania portal.ajira.go.tz na Jinsi ya Kutuma Maombi ya Ajira, Kusajili Katika Tovuti ya Kuajiri Watumishi Mbalimbali nchini Tanzania, Ajira na Jinsi ya Kujisajili katika Mfumo wa Ajira Tanzania.
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (PSRS) ni chombo cha Serikali chenye hadhi ya Idara inayojitegemea iliyoanzishwa mahususi kuwezesha mchakato wa Kuajiri Watumishi katika Utumishi wa Umma.
Ajira Portal ni mfumo ulioanzishwa na Serikali kwaajili ya kuchakata kwa urahisi Utangazaji na kuajiri watu katika Utumishi Wa Umma.
Zifuatazo ni hatua za kufuata ili kujisajili katika Ajira Portal (UTUMISHI).
Aidha unaweza kutazama matangazo na kuomba ajira zinazotangazwa na sekretarieti husika Kwa kufuata hatua zifuatazo;

JINSI ya Kujisajili na Kutuma Maombi ya Kazi Kupitia Ajira Portal
- Bonyeza RECRUITMENT PORTAL
- Bonyeza VACANCIES
Chagua Tangazo la ajira unayotaka kuomba kisha bonyeza Login to Apply iliyoko kulia au chini ya tangazo.

JINSI ya Kujisajili na Kutuma Maombi ya Kazi Kupitia Ajira Portal
Kama una-account (umejisajili) Ingiza Email na Password yako kutuma maombi.

JINSI ya Kujisajili na Kutuma Maombi ya Kazi Kupitia Ajira Portal
Jaza taarifa zako vema (Email ambayo unakumbuka password yake), Jaza Password (neno la siri utakalokumbuka kwa urahisi lakini lisiloweza kufikirika kwa urahisi na mtu mwingine)

JINSI ya Kujisajili na Kutuma Maombi ya Kazi Kupitia Ajira Portal
Utapata Ujumbe ufuatao hapa chini
Registration Success
You have successfully registered with Recruitment Portal. An email has been sent to you with instructions on how to activate your account.
Please check your email and follow the instructions in order to start using your account.
Thanks”
Ingia kwenye email yako kisha fuata maelekezo yaliyotumwa huko
Baada ya hayo yote Bonyeza Login to Apply.
Aidha Waombaji wa Ajira mnatakiwa kuhuisha (Update) taarifa zenu kwa kutumia namba ya utambulisho wa Taifa (NIN), kwenye eneo ya Personal Details.
Mnatakiwa kuhuisha taarifa kwenye eneo la Academic Qualification kwa kuweka kozi yako kwenye Category husika.
Ili kuona ‘STATUS’ ya maombi yako ya kazi, ingia sehemu ya ‘MY APPLICATION’ baada ya ku-‘login’ katika akaunti yako.
Sehemu hii itakuwezesha kuona namba ya usaili kwa wale waliofanikiwa na sababu ya kutokuitwa kwa wale ambao hawajafanikiwa.
Jiunge na Watanzania wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini pamoja na Makampuni Mbalimbali.
Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku ni bure kabisa, JIUNGE HAPA
JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.

Tags: How To Open Ajira Portal Account, JINSI ya Kujisajili na Kutuma Maombi ya Kazi Kupitia Ajira Portal