MAGAZETI ya Leo Jumatano 16 April 2025

Filed in Magazeti, Michezo by on April 16, 2025 0 Comments
     

MAGAZETI ya Leo Jumatano 16 April 2025

Bunge limepitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2025/26 huku Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisema Serikali itaendelea kuhakikisha kuna hali ya usalama, amani na utulivu kipindi chote cha uchaguzi.

MATANGAZO YA KAZI BOFYA HAPA

Ofisi hizo zimepitishiwa Sh782.08 bilioni katika mwaka huo wa fedha.

Hotuba hiyo ilichangiwa na wabunge 103 lakini Majaliwa akasema mambo mengi atayatolea majibu kwa maandishi.
Akihitimisha hoja hiyo Aprili 14, 2025, Majaliwa alisisitiza wananchi kujitokeza kwa wingi katika maboresho ya awamu ya pili ya Daftari la Kudumu la Wapigakura ili wapate haki yao kwenye uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika mwisho.

Majaliwa amesema Serikali iko tayari kushirikiana na vyama vya wafanyakazi likiwamo Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), ili wafanyakazi wapate stahiki zao.

Hata hivyo, wakati wa kupitisha vifungu, hakuna mbunge aliyesimama kuhoji jambo lolote, hivyo vimepita kama vilivyoombwa.

Je, Unatafuta Nafasi za kazi?
Jiunge na Watanzania wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini pamoja na Makampuni Mbalimbali.
Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku ni bure kabisa, JIUNGE HAPA

JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.

Tags:

About the Author ()

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *