Magazeti ya Tanzania Leo Ijumaa 14 February 2025
Magazeti ya Tanzania Leo Ijumaa 14 February 2025
Wawakilishi wa Kanisa Katoliki (RC) lenye ushawishi mkubwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), wamekutana na Kiongozi Mkuu wa Muungano wa Waasi (AFC/M23), Corneille Nangaa kujadili namna ya kurejesha amani Mashariki mwa nchi hiyo.
Kikao kilichowakutanisha viongozi hao wa dini na uongozi wa waasi ulifanyika Jumatano Februari 12, 2025, zikiwa zimepita wiki tatu tangu M23 watangaze kuyatwaa maeneo ya Jimbo la Kivu Kaskazini ikiwemo Mji Mkuu wa jimbo hilo, Kivu.
Shirika la Habari la Reuters limeripoti mkutano huo ulifanyika mjini Goma huku kiongozi wa waasi, Corneille Nangaa, akijaribu kujitambulisha kama msemaji wa wanasiasa na makundi ya waasi yanayompinga Rais wa DRC, Félix Tshisekedi.
Kundi la Nangaa, linaloitwa Alliance Fleuve Congo (AFC) na linaloiona M23 kama kitengo chake cha kijeshi, limekuwa likiudhibiti Mji wa Goma, ambao ni Mji Mkuu wa Jimbo la Kivu Kaskazini, tangu mwishoni mwa January.
Jumanne wiki hii, lilitishia kuendeleza mashambulizi kuelekea Bukavu ambao ni Mji Mkuu wa Kivu Kusini.
Je, Unatafuta Nafasi za kazi?Jiunge na Watanzania wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini pamoja na Makampuni Mbalimbali.
Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku ni bure kabisa, JIUNGE HAPA
JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.
