NACTVET Jinsi ya Kuhakiki Udahili wa Vyuo

NACTVET Jinsi ya Kuhakiki Udahili wa Vyuo
NACTVET Jinsi ya Kuhakiki Udahili wa Vyuo
JE! WEWE NI MWANAFUNZI ULIYEDAHILIWA KATIKA VYUO VYA KATI KWA NGAZI YA ASTASHAHADA NA STASHAHADA?
Kama jibu ni ndiyo, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) linakusisitiza kuhakiki udahili wako kwa kufuata hatua zifuatazo;
ili Kuhakiki Udahili wako Ingia kwenye tovuti ya NACTVET www.nactvet.go.tz.
- Bofya link iliyoandikwa “Student Information Verification“.
- Jaza taarifa zako kwa usahihi kadri mfumo utakavyokuelekeza.
- Jiridhishe kuhusu chuo ulichosajiliwa na programu unayosoma.
- Endapo kuna changamoto, tafadhali wasiliana na Afisa Udahili katika chuo chako.
- Tembelea mara kwa mara mfumo huu kuhakiki taarifa zako ikiwemo matokeo ya kila muhula na endapo una changamoto kwenye hali ya matokeo yako, tafadhali wasiliana na Afisa mitihani wa chuo.
Kumbuka Ukamilifu wa taarifa zako kwenye mfumo huu ndiyo utakuwezesha kupata Namba ya Utambuzi wa Tuzo (AVN) pamoja na Hati ya Matokeo
(transcript) baada ya kuhitimu.
Kwa Ufafanuzi Zaidi Piga Bure
0800110388
Jiunge na Watanzania wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini pamoja na Makampuni Mbalimbali.
Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku ni bure kabisa, JIUNGE HAPA
JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.
