RAIS Samia Afanya Uteuzi Mpya 29 January 2025

RAIS Samia Afanya Uteuzi Mpya 29 January 2025
RAIS Samia Afanya Uteuzi Mpya 29 January 2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, walioteuliwa ni kama ifuatavyo:
Jaji Mstaafu Beatrice Rhoda Mutungi ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Rufani za Kodi (TRAT). Jaji Mstaafu Mutungi anachukua nafasi ya Jaji Mstaafu Gad John Mjemmas ambaye amemaliza muda wake;
Dkt. Diwani Bakari Msemo ameteuliwa kuwa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI). Dkt. Msemo ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani, anachukua nafasi ya Dkt. Julius David Mwaiselage ambaye atapangiwa majukumu mengine; na
CPA. David Carol Nchimbi ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya NMB Plc. CPA. Nchimbi anachukua nafasi ya Dkt. Edwin Mhede ambaye ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
TAZAMA AJIRA ZOTE TANZANIA
Je, Unatafuta Nafasi za kazi?Jiunge na Watanzania wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini pamoja na Makampuni Mbalimbali.
Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku ni bure kabisa, JIUNGE HAPA
JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.
