Simba vs Azam FC kupigwa Benjamin Mkapa Stadium 24 February 2025

Filed in Michezo by on February 22, 2025 0 Comments
     
Simba vs Azam FC kupigwa Benjamin Mkapa Stadium 24 February 2025

Simba vs Azam FC kupigwa Benjamin Mkapa Stadium 24 February 2025

Simba vs Azam FC kupigwa Benjamin Mkapa Stadium 24 February 2025

MATANGAZO YA KAZI BOFYA HAPA

BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imebadili uwanja na muda wa kuanza kwa mchezo namba 167 wa Ligi Kuu ya NBC (Simba SC vs Azam FC) ambao ulipangwa kufanyika kwenye uwanja wa KMC Complex February 24, 2025 kuanzia saa 10:00 alasiri.

Mchezo huo sasa utafanyika kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam kuanzia saa 1:00 usiku Februari 24, 2025.

Sababu ya mabadiliko hayo ni kutoa nafasi kwa mashabiki wengi zaidi kuhudhuria mchezo huo ambao ni moja ya michezo mikubwa ya Ligi Kuu ya NBC inayovuta hisia za watu wengi.

Uwanja wa Benjamin Mkapa wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 60,000 umekuwa ukitumika kwa michezo mingi mikubwa na inayohusisha mashabiki wengi zaidi.

Klabu shiriki (Simba na Azam) pamoja na wadau wengine wa mchezo huo wametumiwa taarifa rasmi ya mabadiliko haya na maandalizi yake yanaendelea vizuri yakiwemo mazingatio ya kiusalama.

Bodi inawatakia wadau wote maandalizi mema ya mchezo huo maarufu kwa jina la ‘Mzizima Derby’.

Je, Unatafuta Nafasi za kazi?
Jiunge na Watanzania wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini pamoja na Makampuni Mbalimbali.
Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku ni bure kabisa, JIUNGE HAPA

JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.

Tags:

About the Author ()

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *