TAMISEMI Kutoa Ajira Za Mkataba Kada ya Afya na Elimu 2025

Filed in Ajira by on April 18, 2025 1 Comment
     
TAMISEMI Kutoa Ajira Za Mkataba Kada ya Afya na Elimu 2025

TAMISEMI Kutoa Ajira Za Mkataba Kada ya Afya na Elimu 2025

TAMISEMI Kutoa Ajira Za Mkataba Kada ya Afya na Elimu 2025

MATANGAZO YA KAZI BOFYA HAPA

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-TAMISEMI (Afya) Dkt. Festo Dugange, amezitaka halmashauri zenye uwezo wa kiuchumi kuajiri watumishi wa mikataba ili kutatua changamoto ya upungufu wa watumishi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa

Dkt. Dugange ametoa maelekezo hayo kwa wakurugenzi wa halmashauri nchini, wakati akifunga mkutano wa 15 wa Taasisi ya Maboresho ya Mamlaka za Serikali za Mitaa (TOA) uliofanyika kwa siku mbili katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo kwenye Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

“Ofisi ya Rais-TAMISEMI ilitoa mwongozo maalum wa namna ya kuajiri watumishi wa mikataba na hususani wa sekta ya elimu na afya, hivyo Makatibu Tawala wa Mikoa kawasimamieni Wakurugenzi wa Halmashauri kutekeleza mwongozo huo,” Dkt. Dugange amesisitiza.

Dkt. Dugange amesema, Serikali imeleta fedha nyingi katika halmashauri ambazo zimejenga zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya na shule na inaendelea kuajiri kwa awamu, hivyo halmashauri zinazokusanya mapato ya kutosha zinapaswa kuajiri watumishi wa mikataba ili waweze kutoa huduma kwa wananchi kupitia mbiundombinu hiyo iliyojengwa na Serikali.

Aidha, Dkt. Dugange amehimiza kuwa, siku zote Ofisi ya Rais-TAMISEMI inaamini watumishi wote waliochini ya TAMISEMI wakifanya kazi kwa bidii na ufanisi, ni dhahiri kwamba kiwango cha utendaji kazi wa Serikali kitakuwa ni zaidi ya asilimia tisini kwani majukumu yanayotekezlezwa na TAMISEMI yanawagusa wa Tanzania wengi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tawala za Mikoa wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI Bi. Beatrice Kimoleta amesema kuwa, TAMISEMI itaendelea kushirikiana na Taasisi ya Maboresho ya Mamlaka za Serikali za Mitaa (TOA) ili iweze kuwa imara na kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Je, Unatafuta Nafasi za kazi?
Jiunge na Watanzania wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini pamoja na Makampuni Mbalimbali.
Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku ni bure kabisa, JIUNGE HAPA

JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.

Tags:

About the Author ()

Comments (1)

Trackback URL | Comments RSS Feed

  1. MFAUME ATHUMANI HASSAN says:

    NAOMBA KAZI NITAFANYA KAZI KWA BIDII ELIMU YANGU NI STASHAHADA YA UALIMU SEKONDARI

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *