VIINGILIO Simba vs Stellenbosch 20 April 2025

VIINGILIO Simba vs Stellenbosch 20 April 2025
VIINGILIO Simba vs Stellenbosch 20 April 2025
Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba, Ahmed Ally ametangaza viingilio vya mchezo wa mkondo wa Kwanza wa Nusu Fainali ya kombe la Shirikisho (CAF CC) dhidi ya Stellenbosch utakaopigwa Jumapili ya April 20 kwenye uwanja wa New Amaan Complex
Ahmed ametangaza viingilio hivyo leo visiwani Zanzibar katika Mkutano na waandishi wa habari na kusema kuwa Uwanja wa Amaan unaingiza watu 15,885 tu.
Viingilio vya mchezo huo ambao utapigwa Kuanzia Saa 10:00 jioni ni Tsh 40,000 Kwa VIP A, 20,000 Kwa VIP B na Mzunguko itakuwa ni Tsh 10,000 tu ambapo Tiketi zake zitauzwa kwa mfumo wa N-Card.
Kuanzia hivi sasa tiketi zinapatikana katika maeneo mbalimbali. Kwa wale wa Dar es Salaam vituo vyote ambavyo vinauza tiketi vitaendelea kuuza tiketi kama kawaida.
Kwa Upande wa Zanzibar ambao wamezoea kununua tiketi za karatasi kwasasa wanaweza kununua tiketi za N-Card na ukawa nayo hadi siku ya mchezo.
Siku ya mchezo tiketi hazitauzwa nje ya uwanja na maeneo mengine yataendelea na huo ni Utaratibu wa CAF, hivo yeyote ambaye anahitaji tiketi anunue tiketi sasa.

Vituo vya kununua tiketi za mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Stellenbosch FC ukiwa Zanzibar.
Vituo vya Dar es Salaam pia vinauza tiketi.
Jiunge na Watanzania wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini pamoja na Makampuni Mbalimbali.
Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku ni bure kabisa, JIUNGE HAPA
JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.
