Yanga haiko tayari kucheza na Simba Siku nyingine

Yanga haiko tayari kucheza na Simba Siku nyingine
Yanga haiko tayari kucheza na Simba Siku nyingine
Uongozi wa Young Africans Sports Club umesema kuwa mchezo wao wa Ligi Kuu ya NBC, uliopangwa kuchezwa leo tarehe 8/3/2025, dhidi ya Simba SC, saa 1:15 usiku upo palepale na hakuna mabadiliko yoyote.
Young Africans SC kama wenyeji wa mchezo, wanaamini taratibu zote za mchezo kama inavyoelekezwa kwenye kanuni za Ligi Kuu ya NBC, ziko sawa na maandalizi yote yako tayari.
Uongozi wa Klabu hiyo umesisitiza kuwa utapeleka timu uwanja wa Benjamin Mkapa kama inavyoelekezwa kwenye kanuni, na hautakuwa tayari kucheza mchezo siku nyingine tofauti na leo.
Yanga inawaalika uwanjani Wanachama, Mashabiki, Wapenzi wa Klabu yetu na Wadau wengine waliosafiri kutoka mikoani, nchi za jirani na sehemu mbalimbali duniani kote kuja kushuhudia mchezo huu mkubwa Barani Afrika.
Katika taarifa hii ya Yanga hakuna sehemu inaonesha kukemea tukio walilofanyiwa Simba SC.

Yanga haiko tayari kucheza na Simba Siku nyingine
TAZAMA AJIRA ZOTE TANZANIA
Je, Unatafuta Nafasi za kazi?Jiunge na Watanzania wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini pamoja na Makampuni Mbalimbali.
Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku ni bure kabisa, JIUNGE HAPA
JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.
